Shambulizi la Urusi laua 19 Ukraine, limo lililopiga Kiev

Tangu itangaze kuanza uvamizi wake nchini Ukraine, Urusi imeyatwaa maeneo ya Mkoa wa Donetsk, Lugansk, Kherson, Zaporizhia, Pokrovisk na Crimea iliyochukukiwa na Urusi kutoka Ukraine mwaka 2014.

Apr 6, 2025 - 13:11
Apr 6, 2025 - 13:22
 0  5
Shambulizi la Urusi laua 19 Ukraine, limo lililopiga Kiev
Shambulizi la Urusi laua 19 Ukraine, limo lililopiga Kiev
Shambulizi la Urusi laua 19 Ukraine, limo lililopiga Kiev
Shambulizi la Urusi laua 19 Ukraine, limo lililopiga Kiev

Kiev. Shambulizi lililoletekezwa na Urusi nchini Ukraine limesababisha vifo vya watu 19 huku makumi wakijeruhiwa na kupatiwa matibabu hospitalini.

 Miongoni mwao ni waliojeruhiwa katika mashambulizi ya anga ya Urusi katika jiji la Kyiv nchini Ukraine pamoja na kusini mwa Ukraine baada ya Rais, Volodymyr Zelenskyy kuikosoa Marekani kwa kuitikia kwa “udhaifu” shambulio lililoua watu 19 katika mji wake wa kuzaliwa, wakiwemo watoto tisa.

 Shirika la Habari la Associated Press limeripoti leo Jumapili Aprili 6,2025, kuwa Meya wa Jiji la Kyiv, Vitali Klitschko, amesema mashambulizi ya anga dhidi ya mji mkuu wa Kyiv mapema Jumapili yalisababisha moto katika majengo yasiyo ya makazi katika wilaya tatu na kujeruhi watu watatu.

 Kwa upande mwingine, Vitaliy Kim, ambaye ni Gavana wa Mkoa wa Mykolaiv Kusini mwa Ukraine, alisema Urusi ilirusha kombora majira ya saa nne usiku Jumamosi, na kusababisha uharibifu wa nyumba kadhaa na kuwajeruhi watu wanne.

 Nchi nzima iliwekwa chini ya tahadhari ya anga kuanzia saa nane usiku baada ya jeshi la anga la Ukraine kutoa onyo la shambulio, ikiwa ni pamoja na maeneo ya mpakani na Poland, jambo lililosababisha mwanachama huyo wa NATO kurusha ndege angani kwa ajili ya usalama wa anga.

 Jeshi la Poland lilisema jeshi lake pamoja na majeshi ya washirika walipanda anga “kutokana na shughuli nyingi za anga ndefu za Shirikisho la Urusi” upande wa magharibi mwa Ukraine, huku mifumo ya ulinzi wa anga ya ardhini ikiwa kwenye hali ya tahadhari kubwa.

 “Hatua zilizochukuliwa zinalenga kuhakikisha usalama katika maeneo ya mipakani yanayokabiliwa na hatari.”

 Jeshi la anga la Ukraine lilisema siku ya Jumapili kuwa mifumo yao ya ulinzi wa anga ilidungua makombora 13 kati ya 23 na droni 40 kati ya 109 zilizoanzishwa na Urusi katika shambulio la usiku.

 Liliongeza kuwa droni 53 zilipotea, likimaanisha jeshi la Ukraine lilitumia mbinu za kivita za kielektroniki kuzielekeza droni hizo mahali pengine.

 Wizara ya Ulinzi ya Urusi ilisema droni 11 za Ukraine zilidunguliwa usiku kucha katika maeneo ya Kursk, Belgorod na Rostov.

 Ijumaa, shambulio la Urusi katika mji wa Kryvyi Rih liliua angalau watu 18, wakiwemo watoto wadogo hadi wa miaka mitatu.

 Kombora la Urusi lilipiga eneo la makazi karibu na uwanja wa michezo katika mji wa kati wa Ukraine.

 Katika taarifa ya hisia kali kwenye mitandao ya kijamii, Zelenskyy alitaja majina ya watoto tisa waliouawa katika shambulio hilo kwenye mji wake wa kuzaliwa, huku akiikosoa ubalozi wa Marekani kwa kile alichokiita “taarifa dhaifu.”

 Balozi wa Marekani, Bridget Brink, alichapisha ujumbe kwenye X siku ya Ijumaa akisema alikuwa “ametishwa” na shambulio hilo, bila kuitaja Urusi kama mshambuliaji.

 “Kwa bahati mbaya, mwitikio wa ubalozi wa Marekani umekuwa wa kushangaza kwa njia isiyopendeza: taifa lenye nguvu, watu wenye nguvu lakini majibu dhaifu kama haya,” aliandika Zelenskyy.

 Oleksandr Vilkul, mkuu wa utawala wa kijeshi wa Kryvyi Rih, alisema siku tatu za maombolezo zimetangazwa kuanzia Aprili 7.

 Mashambulizi hayo yamekuja wakati Rais wa Marekani, Donald Trump, anasukuma pendekezo la kusitisha mapigano kwa sehemu kati ya Urusi na Ukraine, zaidi ya miaka mitatu tangu Urusi ianze uvamizi wake mkubwa.

 Zelenskyy alisema shambulio dhidi ya Kryvyi Rih linaonyesha kuwa Urusi haina nia yoyote ya amani.

What's Your Reaction?

Like Like 0
Dislike Dislike 0
Love Love 0
Funny Funny 0
Angry Angry 0
Sad Sad 0
Wow Wow 0